Sunday, August 29, 2010

078

078

Hakuna kitu chochote duniani laini kama maji unapoyashika.

Lakini unapotaka kulainisha vigumu na visivyokunjika hakuna zana bora kama maji kwa kazi kama hiyo.

Laini hushinda kigumu;
na mororo hushinda kilichokakamaa.
Kila mtu anajua hili ni kweli; lakini wachache sana wanaoweza kulifanza hili kwa matendo.

Kwa sababu hii ndiyo maana gwiji huwa mtulivu wakati wa majonzi.

Ushetwani hauingii moyoni mwake.
Kwa kuwa alishaghairi kusaidia, basi huwa ndiye msaada mkubwa kabisa kwa watu.

Maneno haya budi yanaonekane yanayojikinza. [Kwa wasiojua].


AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]


Copyright © Sammy Makilla-2010

No comments:

Post a Comment