076
Watu huzaliwa teketeke na laini;
Wafu, ni wagumu na waliokakamaa.
Mimea huzaliwa mororo na inayojikunja;
Ikinyauka, huwa inasagika na kavu.
Kwa hiyo yeyote anayekakamaa na kutokunjika ni mfuasi wa mauti.
Yeyote anayelainika na kuteleza ni mfuasi wa uhai.
Kilicho kigumu na kilichokakamaa kitavunjika.
Kilicho kilaini na teketeke kitadumu daima dawamu.
AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]
Copyright © Sammy Makilla-2010
Sunday, August 29, 2010
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment