Sunday, August 29, 2010

081

Maneno ya kweli si fasaha; na maneno fasaha si kweli.
Wenye busara hawahitaji kuthibitisha hoja zao; na watu wanaohitaji kuthibitisha hoja zao sio watu wenye busara.

Gwiji hana anachomiliki.
Kadri anavyowafanyia wengine hisani zaidi ndivyo anavyofurahi zaidi.
Kadri anavyowapa wengine, ndivyo anavyozidi kuwa tajiri.
Tao hulisha bila kulazimisha.
Bila kuwa mtawala wa kiimla, gwiji huongoza.

AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]

No comments:

Post a Comment