01
Tao inayoweza kuelezewa siyo Tao ya milele.
Jina linaloweza kutajwa kama jina sio jina la milele.
Kisichowezekana kupewa jina ndicho kilicho milele, cha kweli.
Kupewa jina ndio mwanzo wa vitu vyote vilivyopo ulimwenguni.
Huru kutokana na matamanio
huigundua ajabu hii.
Ukidakwa na matamanio basi utakachokiona ni vitu vinavyoonekana kwa nje tu.
Lakini ajabu na dalili za kuwepo ni vitu vinavyoanzia kwenye chanzo kimoja.
Chanzo hicho huitwa giza.
Giza ndani ya giza,
lango kuu kuingia kwenye uelewa wa kila jambo.
AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]
Tuesday, September 7, 2010
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment