Tuesday, September 7, 2010

03

03
Ukiwaheshimu watu wakubwa kupita kiasi au kupindukia,
Watu hukosa nguvu na uwezo.

Ukizipa mali thamani kuliko watu,
basi watu huanza kuiba na kuwa wezi.

Mwalimu huongoza kwa kupakua kwanza akili za watu zikabakia tupu,
na kisha huanza kujaza akilini
kwa kudhibiti matamanio yao na kuamsha utu, ubinadamu na hamasa zao.
Huwasaidia watu kupoteza kila kitu wanachojua, wanachokitamani na kuzusha kuchanganyikiwa miongoni mwa wale wanaodhani wanajua.

Anza kufanya mazoezi ya kutofanya kitu chochote na kila kitu kitajiendesha chenyewe kwa asili bila kasoro.

AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]

No comments:

Post a Comment