Tao haihesebaki, haina idadi na ni isiyo na mwisho.
Kwanini haina mwisho na haifi ?
Haina mwisho na haifi kwa sababu haikuzaliwa;
kwa hiyo haiwezi ikafa.
Kwanini haihesabiki ?
Haina matamanio ya kujinufaisha yenyewe;
Kwa hiyo ipo kwa ajili ya kila kiumbe duniani.
Mwalimu siku zote hubakia nyuma;
Na ndio sababu siku zote yuko mbele ya wengine.
Hujitenga na vitu vyote;
Na ndio sababu yeye na hivyo vitu vingine ni kitu kimoja.
Kwa sababu amejiachia kwa vitu vyote,
huwa hana anachokikosa.
AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]
Tuesday, September 7, 2010
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment