Tuesday, September 7, 2010

02

Wakati watu wanapoona baadhi ya vitu kama vinavyopendeza;
vitu vingine huonekana vinavyochukiza na vibaya.
Watu wanapoona vitu vingine ni vizuri,
basi vingine hugeuka vyenye sura mbaya.

Kuwa na kuwepo ni vitu viwili vinavyoumbana;
Ugumu na urahisi wa mambo ni vitu vinavyoungana mkono;
Refu na fupi hufafanuana;
Juu na chini hutegemeana;
Kabla na baadaye hufuatana.

Kwa hiyo mwalimu hufanza bila kufanya kitu chochote
na hufundisha bila kusema chochote.
Vitu huzuka na huviachia vije,
Vitu hutoweka na huviachia kwenda zake.
Huwa navyo lakini hamiliki,
hufanya mambo bila kutarajia chochote.
Na kazi yake ikishafanyika huisahau.
Ndio sababu kazi zake hudumu milele.


AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]

No comments:

Post a Comment