Njia hii kuu ni rahisi,
hata hivyo watu hupendelea vichochoro.
Tambua ni wakati gani mambo hayana ulingano. Jitahidi uwe katikati mwa Tao.
Walanguzi matajiri wanaponeemeka
Wakati wakulima wanadhulumiwa ardhi yao;
wakati maofisa serikali wanapotumia fedha kununua silaha badala ya kununua dawa;
wakati tabaka la juu ni wabadhirifu na mafisadi na masikini hawana pa kukimbilia-haya yote ni wizi na rabsha.
Huu kamwe si mwenendo unaoendana na Tao.
AYA ZA MTAWA
[ Tao-Te-Ching ]
Copyright © Sammy Makilla-2010
Sunday, September 5, 2010
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment